VIDEO: Rais Magufuli aipongeza Stars kwa kufuzu
newsare.net
Dar es Salaam. Rais John Magufuli ameipongeza timu ya Taifa kwa kufuzu kucheza fainali za michuano ya Afrika mwaka 2019 baada ya leo Jumapili Machi 24, 2019 kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Uganda. Taarifa iliyotolewa leo na Mkurugenzi wa MawasilianoVIDEO: Rais Magufuli aipongeza Stars kwa kufuzu
Dar es Salaam. Rais John Magufuli ameipongeza timu ya Taifa kwa kufuzu kucheza fainali za michuano ya Afrika mwaka 2019 baada ya leo Jumapili Machi 24, 2019 kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Uganda. Taarifa iliyotolewa leo na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa inaeleza kuwa kiongozi mkuu huyo wa nchi alifuatilia mchezo huo uliochezwa Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam kupitia televisheni. “Rais alikuwa akifuatilia pambano hilo kupitia luninga amerekodiwa picha ya video akifurahia ushindi baada ya pambano la Taifa Stars na Uganda kumalizika kwa Taifa Stars kupata ushindi wa magoli matatu kwa sifuri,” inaeleza taarifa hiyo. Rais Magufuli amesema ushindi huo ni heshima kwa nchi na kuwapongeza Watanzania wote kwa ushindi huo, ikiwa ni miaka 39 tangu Tanzania iliposhiriki michuano hiyo mwaka 1980. Magoli ya Taifa Stars yalifungwa na Saimon Msuva, Erasto Nyoni na Aggrey Morris. Read more